Magonjwa ya kuambukia ni nini?
Jifunze kila kitu kuhusu nini inafanya ugonjwa kuwa wa kuambukia, wapi unatoka na ni magonjwa gani ya kuambukia ni ya kawaida katika maeneo ambapo VAW na I&I wanapatikana.
Ugonjwa wa kuambukia ni nini?
Magonjwa ya kuambukia ni magonjwa inayo sababishwa na viumbe vinavyo itwa patojeni ambavyo vinaleta magonjwa ndani ya jamii zetu. Iyi magonjwa inaweza kusambalana kutoka kwa mazingira yetu ikiwemo chakula ao maji, kutoka kwa wanyama na bidudu bingine ao kutoka kwa watu wengine ambao wanaweza kuwa ni wagonjwa tayari. Alama na dalili zinaweza kutofautiana kulingana na ukali wa maambukizi. Kuna wakati magonjwa hayo inaweza kutunzwa kwa kupumuzika ao kwa kutumia dawa, na wakati ingine inaweza hitajika kwenda ku hospitali.
Patojeni ni nini?
Patojeni ni viumbe vidogo ambavyo vina ambukiza chanzo yenye kuwa hai kama vile wanadamu na inatumia viungo vya chanzo ili kuongezeka na kusababisha ugonjwa. Aina ine kuu za patojeni ni virusi, bakteria, shampinyo na parazite. Kwa kawaida, mfumo wetu wa kinga unaweza kutulinda na maambukizi inayo sababishwa na patojeni, lakini hata hivyo, kuna wakati patojeni zinaweza kuzidia nguvu kinga yetu ya mwili na kusababisha ugonjwa ambayo inapashwa kutunzwa. Patojeni zinaweza kusambalana katika jamii zetu kupitia njia mingi tofauti.
Aina za patojeni
Aina tofauti za patojeni zinasababisha aina tofauti za magonjwa. Hizi ni mifano za magonjwa yanayo sababishwa na kila aina ya patojeni:
-
Virusi
Virusi ni chembe ndogo sana na inaundwa na ADN ya kinga yenye kuwa na proteine. Virusi vinahitaji chanzo yenye kuwa hai ili kuongezeka na kusababisha magonjwa mingi ya kawaida ya kuambukia ambayo tunaona katika jamii zetu. Magonjwa inayo sababishwa na virusi ni pamoja na mafua, homa ya kawaida, suluba, fievre jaune, biharagabo ao varicelle, ugonjwa wa maini na COVID-19.
-
Bakteria
Bakteria ni viumbe vidogo sana. Katika hali ya kawaida, wanadamu tuna bakteria nzuri katika mwili yetu ambazo zinasaidia mwili yetu kutumika muzuri. Hata hivyo, kuna bakteria pia zinazo sababisha magonjwa ambayo inaweza kukufanya ugonjwe. Hizi bakteria zinaweza kusababisha magonjwa kama vile kifua kikuu, kipindupindu, kivimba ya koromeo, fievre tifoide, maambukizi ya njia ya mukoyo na tetanose.
-
Parazite
Parazite ni viumbe ambavyo vinaishi mbali na vyanzo (hotes) na mara mingi vinapatikana katika chakula na maji ya buchafu ao kwa kulumwa na vidudu. Parazite zinatumia viungo vya vyanzo vyayo kama vile malisho ili kwendelea kuongezeka, hali ambayo inaweza kusababisha ugonjwa wakati parazite inatowa sumu katika mwili yetu. Mfano ya magonjwa yanayo sababishwa na parazite ni malaria, ugonjwa wa usingisi ao maladie du someil na upele.
-
Shampinyo
Shampinyo ni viumbe vidogo kama vile chachu na ukungu ambazo zinazoweya kupatikana mu hewa yenye tunapumua, kwenye ngozi yetu ya mwili na kwenye mimea na udongo. Aina zingine za kipekee za shampinyo zinaweza kusababisha ugonjwa hasa kwa watu wenye kuwa na mfumo zaifu wa kinga ya mwili. Magonjwa ya kawaida ya shampinyo ni pamoja na homa ya uti ao menenjite, bishekera ao teigne na vidonda ndani ya tumbu ao kinywa.
Maelezo zaidi kuhusu magonjwa ya kuambukia katika maeneo ya mikutano.
Aina zingine za magonjwa
Magonjwa yote siyo ya kuambukia. Aina zingine za magonjwa ambayo unaweza kuona kwenye mazingira ya kuishi ya mkutano ni pamoja na:
Namna mtu anaishi: namna yetu ya kuishi inaweza kuwa na vinyume kwenye afya yetu. Kujuwa kile tunacho kula, kiasi cha mazoezi (sport) na kushiriki katika shuruli ambazo zinatufanya kusikia furaha inaweza kuwa na matokeo makubwa kwa afya yetu ya kimwili na ya akili. Hiyi inaweza kusaidia kupunguza hatari ya magonjwa mingi kama vile ugonjwa wa moyo na mishipa, ugonjwa wa kisukari, ugonjwa migulu (arterite) na aina mbalimbali za kansere.
Bisanya na Vidudu: Bisanya ao kunguni habisababishi maambukizi lakini binaweza sababisha ngozi yetu kuwashwa wakati binatuluma na inaweza kuwa vigumu kubiuwa byote. Fanya usafi muzuri ndani ya nyumba yote, fula shuka za kitanda mara kwa mara na safisha fasi yenye unaishi. Uchunguzi wa mara kwa mara wa bisanya ndani ya nyumba yako inaweza pia kusaidia kutambua mapema uvamizi wa bisanya na kuhakikisha habiendeleyi naongezeka. Tafazali angalia section ya habari kuhusu vifaa vya kuelemisha.
Kufasiria watoto kuhusu magonjwa ya kuambukia
Inaweza kuwa vigumu kufasiria watoto maneno ya kipekee kuhusiana na mikrobe na gisi maambukizi inasambalana. Zaidi ya hiyo, inaweza kuwa vigumu kuwafasiria sababu gani tunapashwa kufunika mdomo yetu wakati tunakohola ao kunawa mikono yetu mara kwa mara! Jisikie huru kuchunguza Eneo ya Watoto ili kupata vifaa vya kuelemisha ambavyo vinaweza kusaidia kufundisha watoto kuhusu hatua na mbinu ambazo wanaweza kutumia ili kujilinda na magonjwa ya kuambukia.